
Mchezaji mpya wa Manchester City, Gabriel Jesus, amechochea ushindi wa Brazil kwa kufunga magoli mawili na kumpatia kocha mpya wa Brazil Tite ushindi wake wa kwanza katika mchezo dhidi ya Ecuador.
Katika mchezo huo uliochezwa eneo lililo juu kwa futi 10,000 kutoka usawa wa bahari, Brazil iliibuka na ushindi wa magoli 3-0 huku mchezaji nyota wa Brazil Neymar akifunga goli kwa mkwaju wa penati.

Gabriel Jesus licha ya kufunga magoli mawili pia alisaidia kupatikana penati iliyofungwa na Neymar

Neymar akishangilia baada ya kufunga goli la mkwaju wa penati
Post a Comment