
Rais wa Rwanda Paul Kagame, (wa pili kulia) akiwa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, (wa kwanza kulia), akimkabidhi tuzo ya mwoneshaji bora kwenye kategori ya habari, machapisho, uchapishaji na vifaa vya ofisini, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez, wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya 40 ya Biashara ya
Kimataifa ya Dar es Salaam kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam Julai 1, 2016. Wapili kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mh. Charles Mwijage.

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakiwa na tuzo ya ushindi katika banda lao. Kulia Felister Bwana wa Shirika la UNFPA Tanzania, Didi Nafisa (wa pili kulia) pamoja na Hoyce Temu (kushoto).

Post a Comment