
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa
Woinde shizza,Arusha
SERIKALI ya awamu ya tano imesema kuwa itaendeleza jitihada za kutunza na kulinda urithi wa dunia ikiwemo kutoa elimu kwa wananchi wanaoishi maeneo ya uhifadhi ili watanzania wote waweze kunufaikana rasilimali za nchi .
Hayo yalisemwa na waziri mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa akifungua mkutano wa kulinda urithi wa dunia wa Afrika kama nyenzo ya maendeleo
endelevu unaoendelea jijini Arusha
Majaliwa alisema kuwa rasilimali zilizopo ni za watanzania na ili kuhakikisha kuwa wananufaika nazo serikali itahakikisha inatunza na kulinda uhifadhi ili yawe endelevu na kusaidia vizazi vijavyo.
Alisema kuwa Tanzania ni moja ya nchi tajiri yenye urithi na hivyo ili kuhakikisha kuwa wananchi wananufaika haswa waishio maeneo ya uhifadhi
serikali itatoa elimu ya kutosha ili waepuke kuchangia uharibifu wa mazingira
unaotokea kwenye hifadhi za taifa .
“Rasilimali hizi ni zetu na hivyo hata wanaoishi maeneo ya hifadhi
watusaidie kwa wale wanaoingilia na kuharibu kwani hata hizo mali asili zinatusaidia sote na ndiyo sababu tumewekea mikakati ya kutunza maeneo
hayo ili yawe endelevu’alisema
Kwa upande wake mwenyekiti wa mkutano huo ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Mali asili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi Alisema kuwa
madhumuni ya mkutano huo ni kutambua changamoto na mambo ambayo
yanatishia na kuathiri uhifadhi bora wa maeneo ya urithi wa dunia katika afrika .
Woinde shizza,Arusha
SERIKALI ya awamu ya tano imesema kuwa itaendeleza jitihada za kutunza na kulinda urithi wa dunia ikiwemo kutoa elimu kwa wananchi wanaoishi maeneo ya uhifadhi ili watanzania wote waweze kunufaikana rasilimali za nchi .
Hayo yalisemwa na waziri mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa akifungua mkutano wa kulinda urithi wa dunia wa Afrika kama nyenzo ya maendeleo
endelevu unaoendelea jijini Arusha
Majaliwa alisema kuwa rasilimali zilizopo ni za watanzania na ili kuhakikisha kuwa wananufaika nazo serikali itahakikisha inatunza na kulinda uhifadhi ili yawe endelevu na kusaidia vizazi vijavyo.
Alisema kuwa Tanzania ni moja ya nchi tajiri yenye urithi na hivyo ili kuhakikisha kuwa wananchi wananufaika haswa waishio maeneo ya uhifadhi
serikali itatoa elimu ya kutosha ili waepuke kuchangia uharibifu wa mazingira
unaotokea kwenye hifadhi za taifa .
“Rasilimali hizi ni zetu na hivyo hata wanaoishi maeneo ya hifadhi
watusaidie kwa wale wanaoingilia na kuharibu kwani hata hizo mali asili zinatusaidia sote na ndiyo sababu tumewekea mikakati ya kutunza maeneo
hayo ili yawe endelevu’alisema
Kwa upande wake mwenyekiti wa mkutano huo ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Mali asili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi Alisema kuwa
madhumuni ya mkutano huo ni kutambua changamoto na mambo ambayo
yanatishia na kuathiri uhifadhi bora wa maeneo ya urithi wa dunia katika afrika .
Post a Comment