0


Mtu anayedaiwa kuwa ni gaidi wa kundi la al-Shabaab amepigwa risasi na kufa baada ya kumchoma kisu askari wa kikosi cha GSU nje ya ubalozi wa Marekani uliopo eneo la Gigiri Jijini Nairobi nchini Kenya.

Ubalozi wa Marekani umethibitisha kutokea kwa tukio hilo jana, ambapo hakuna mtumishi wa ubalozi huo aliyejeruhiwa, na kuviagiza vyombo vya habari kupata taarifa zaidi kwa serikali ya Kenya.


Mtuhumiwa huyo wa ugaidi inadaiwa kuwa alikuwa akilazimisha kungia kwenye Ubalozi wa Marekani nandipo alipozuiwa na maafisa polisi wa Kenya kwenye geti na kisha alichomoa kisu na kumchoma askari polisi kabla ya kupigwa risasi na kufa.
Maafisa wa upelelezi wa Marekani wa kikosi cha FBI wakiuchunguza mwili wa mtu aliyeuwawa

Post a Comment

 
Top